Friday, July 4, 2014

KOCHA WA BRASIL AMWALIKA MWANASAIKOLOJIA KUSAIDIA WACHEZAJI

Kocha wa Brasil Philip Scolari amemwalika Mwanasaikolojia, Regina Brandao ili asaidie Wachezaji kupambana na msongo wa mawazo unaotokana na kutakiwa kushinda mchezo wao wa Robo Fainali na timu ya Colombia. Hili linatokana na ukweli kuwa timu ya Brasil ambayo ni timu mwenyeji kucheza mbele ya mashabiki ambao lengo lao ni ushindi, ni vigumu. Akizungumza na Shirika la Habari AFP Neymar alisema hajawahi kukutana na jambo kama hili (Kombe la Dunia)na kuwa anafurahi sana. Alisema "ni sisi tu tunaocheza ndio tuna msongo wa mawazo kwa wakati wote wa pambano hivyo kupata mtaalamu wa saikolojia itatusaidia" alimaliza.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.