Sunday, March 8, 2015

MSINGI MATOKEO MAKUBWA SASA NI NIDHAMU




Taifa kwa sasa liko katika vuguvugu la Matokeo Makubwa Sasa ikiwa ni msukumo wa Serikali ya Awamu ya Nne kuhakikisha sekta zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja mfano maji, afya, elimu, usafirishaji na kilimo sinaangaliwa kwa jicho la pekee na Serikali.

Upande wa elimu, msukumo umewekwa katika kuongeza udahili hasa wa wanafunzi wa sayansi ili kubabiliana na upungufu wa wataalamu wa fani mbalimbali wa fani za sayansi.

Katika kuhakikisha hilo, jamii kupitia asasi, mashirika ya dini, Serikali zinatakiwa kuweka msisitizo wa ujenzi wa miundombinu yenye uwezo wa kuzalisha wahitimu wenye uwezo wa kupambana na changamoto za kiutafiti, na kiutekelezaji katika fani hizo za sayansi

Lakini pamoja na utekelezaji wa mipango na mikakati mingi ya kuhakikisha mafanikio yanapataikana, msingi imara katika mafanikio hayo ni nidhamu.

Hilo limedhihirishwa na matoke ya Kidato vidato vya Nne na  Sita katika shule zilizo chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, mathalani kwa shule zilizo chini ya Jeshi la Kujenga Taifa; Jitegemee na Kawawa Sekondari. Matokeo ya Shule yameonesha pamoja na kuwa na miundombinu na walimu wenye uwezo, dhana ya nidhamu ni muhimu katika kufundisha na kujifinza.

Matokeo hayo ambayo Shule ya Sekondari Kawawa (JKT) imefaulishwa kwa 100% na Jitegemee 97.2% yamedhihirisha namna shule hizi zilivyodhamiria kuwa shule bora hapa nchini, na kuwa tegemeo kwa Taifa.
 
Kwa upande wa Jitegemee (JKT) Sekondari, mwanafunzi anapojiunga na shule anapitia mafunzo ya Kwata na kwa ujumla ukakamavu. Mafunzo haya hutolewa kwa wanafunzi wapya wa Kidato cha Kwanza na Tano na wahamiaji katika vidato vingine.

Mafunzo haya yamesaidia  sasa wanafunzi kujenga utayari wa kujitunza hasa katika utimamu wa mwili na akili, utayari wa kupokea maelekezo  na maarifa katika ujifunzi, na kwa jumla nidhamu ya kutambua wajibu wa kila mwanafunzi katika kutumia maarifa anayopata kwa ajili yake, na jamii inayomzunguka.

Jitegemee na Kawawa sekondari zimekuwa ni alama ya ufanisi wa Jeshi la Kujenga Taifa katika eneo la utoaji elimu bora. Shule hizi zimekuwa na sifa ya pekee katika malezi na mafanikio ya wahitimu wake baada ya kuhitimu masomo yao kwani wameajiriwa na kujiajiri katika serikali kuu, sekta ya umma na binafsi.

Mfano Waheshimiwa Jerry Slaa (D) Mstahiki Meya wa Ilala, Mhe. Lucy Mayenga Mkuu wa Wilaya, Mhe. Neema Mgaya Mbunge; wasanii kama Marehemu Kanumba, Kajala, Temba (Mhe. Temba), Ras Pompi Du, wacheza mpira maarufu kama Ally Mayai Tembele, Renatus Njohole (anayecheza nje ya nchi) na wengine wengi waliohitimu Jitegemee.

Msingi wa mafanikio ni nidhamu ambayo imesimamiwa vyema na Menejimenti ya Shule, walimu, wafanyakazi wasio walimu, Serikali ya Wanafunzi, wanafunzi wenyewe na kwa ujumla mfumo bora wa Jeshi la Kujenga Taifa, wa kuratibu na kusimamia utendaji na utekelezaji wa majukumu kwa viongozi wote walio katika nafasi mbalimbali ndani ya Jeshi hilo.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.