Friday, July 4, 2014

MTANANGE WA BRASIL NA COLOMBIA

Leo ni leo katika Mtanange kati ya Timu ya Taifa za Brasil na Colombia. Hili linatokana na ukweli kuwa timu hizi ziko ukanda mmoja, na wanacheza mpira kidago unaofanana. Tofauti itakuwa katika ukweli kuwa Brasil inatakiwa kushinda ili kuwafanya watu wa Brasil ambao hivi karibuni wamekuwa katika maandamano makubwa kupinga gharama kubwa za maandalizi ya kombe hilo, angalau waendelee kuwa watulivu. Timu hizo zinategemea kutumia mifumo: Brasil 4-2-3-1 Cesar; Alves, Silva, Luiz, Marcelo; Fernandinho, Gustavo; Hulk, Oscar, Neymar; Fred. na Colombia: 4-4-2 Ospina; Zúñiga, Zapata, Yepes, Armero; Cuadrado, Aguilar, Sanchez, Rodríguez; Gutiérrez, Martínez. Huku mwamuzi akiwa Carlos Velasco Carballo kutoka Spain

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.